Tuesday, March 25, 2014

Rais wa Al Ahly akamatwa kwa rushwa

Rais wa timu ya Al Ahly Hassan Hamdi amekamatwa na kusekwa ndani akikumbana na mashtaka ya rushwa.

Hamdi alikamatwa Jumapili na ataendelea kubakia rumande kwa siku 15 ili asiweze kutoroka Misri mpaka uchunguzi utakapokamilika.

Hamdy amekataa madai yote anayohusishwa nayo.

Hassan Mahmoud Hamdi Ismail alizaliwa 1949 ni mwenyekiti wa 13 wa wakali hao wa Misri na mwenyekiti wa Al-Ahram advertising agency ambayo ni sehemu ya Al-Ahram Association .

Hamdi ambaye alicheza Al Ahly kama beki tokea mwaka 1969 mpaka 1978 alipata URais wa klabu hiyo mwaka 2002 baada ya mwenyekiti wa zamani Saleh Salim kufariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.