Wednesday, March 26, 2014

Bayern bingwa Bundesliga,waweka rekodi,Guardiola mkali wa mataji

Bayern Munich wamechukua taji lao la 24 la ligi kuu ya Ujerumani Bundesliga huku wakiweka rekodi ya kuchukua ubingwa mapema zaidi baada ya kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Hertha Berlin ikimfanya Pep Guardiola kuchukua taji akiwa na mechi 7 mkononi.

Ikiwa ni msimu wake wa kwanza, Guardiola sasa ameshinda mataji matatu katika miezi tisa Uefa Super Cup,Club World Cup na hilo la ligi.

Kiungo Toni Kroos alifunga bao la kwanza akimalizia kazi nzuri ya Thomas Muller kabla ya
Mario Gotze kutyupia la pili kwa kichwa akimalizia krosi ya Bastian Schweinsteiger.

Franck Ribery akatupia la tatu huku Hertha Berlin bao la machozi likifungwa kwa penati na Adrian Ramos.

Ushindi huo unaifanya Bayeri kufikisha pointi 77 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote.




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.