Wednesday, March 26, 2014

Inter Milan yamuweka kwenye rada Sagna

Inter Milan wanataka kumnasa beki wa Arsenal Bacary Sagna wakati mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu.

Wakali hao wa Italia wamekataa kuwa katika makubaliano na beki wa Manchester United Patrice Evra.

Rais wa Inter Milan Erick Thohir amesema wanataka kumsainisha Sagna kwakuwa wanataka kuweka uwiano wa timu kwakuwa kwasasa wana Yuto Nagatomo na Jonathan kama mmoja akiumia unahitaji mtu mwingine.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.