Wednesday, July 23, 2014

Mourinho atangaza utawala EPL


Kocha Jose Mourinho amesema anataka kuutawala msimu mpya na kuweka mipango ya utawala kwa muda wa muongo mmoja.

Boss huyo wa Chelsea na kikosi chake leo wanashuka dimbani katika maandalizi ya kabla ya msimu kucheza na RZ Pellets huko Klagenfurt, Austria.

Wachezaji waliosajiliwa wakati wa dirisha la usajili linaloendelea Diego Costa, Cesc Fabregas na Filipe Luis tayari wamejiunga na timu hiyo.

Mourinho amesema kama hatafikiri kuwa watashinda taji la EPL ni vyema akarudi nyumbani na kumuacha kocha mwingine kuchukua mikoba hiyo.

Anasema msimu uliopita waliishia nusu fainali ya Champions League ilikuwa ni kipindi cha mpito.

Anaongeza kuwa timu hiyo imekuwa timu ya ushindani kwa miaka 10 ikipitia katika hatua mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.