Monday, May 26, 2014

Chelsea yatumbukia kwa Lavezzi,PSG wawataka Oscar,Hazard na Cech


Chelsea wametumbukia kumtaka mshambuliaji wa Paris St Germain Ezequiel Lavezzi.

Klabu hiyo ya Ufaransa imemsaini beki David Luiz na inaonesha nia ya kuwataka Eden Hazard, Oscar na Petr Cech.
Inafahamika kuwa Chelsea nao wameulizia bei ya Lavezzi ambaye ana kiu ya kucheza kwenye ligi ya kiushindani Zaidi.

Chelsea wanatazama kuimarisha safu yake ya ushambuliaji Samuel Eto'o amemaliza mkataba wake huku pia ikiwa tayari imekubaliana na Atletico Madrid kumsajili mshambuliaji wake Diego Costa.
Jose Mourinho pia anataka kuwapora Manchester City beki Eliaquim Mangala kutokea FC Porto ambaye yupo karibu kutua City huku pia ikimtaka Raphael Varane wa Real Madrid.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.