Tuesday, May 20, 2014

Mandzukic,Guardiola kimenuka


Mario Mandzukic anaelekea kucheza soka huko England,na anaweza kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na kocha mpya wa Manchester United Louis Van Gaal baada ya kubwatukiana na kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola.

Arsenal na Chelsea wanaongoza katika mbio za kumnasa mshambuliaji huyo mwenye miaka 27 kapo United nao wanataka kutumbukia katika mbio za kumnasa.

Mandzukic anaondoka kwa mabingwa hao wa Bundesliga akielezea wazi kutoridhishwa na muelekeo wa na mbinu za Guardiola na tayari kocha huyo amemtakia kila la kheri kusaka maisha mapya kwenye klabu nyingine.

Guardiola hakumuweka kikosini mchezaji huyo kwenye mchezo uliopita walioichapa Borussia Dortmund 2-0 Jumamosi iliyopita katika kombe la Ujerumani licha ya kuwa hakuwa mgonjwa.

Kocha huyo baada ya kujihakikishia kikosi ambacho kingecheza mchezo huo siku ya Alhamis alimfuata Mandzukic,na kumwambia amemtema kwenye kikosi kitakachocheza mchezo huo na akamtakia kila la kheri na klabu yake mpya.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.