Tuesday, December 24, 2013

Mtawala aachia ukatibu Simba,atambulishwa TFF leo

Aliyekuwa katibu mkuu wa Wekundu wa Msimbazi Simba Evodius Mtawala ameachana na klabu hiyo baada ya kupata kazi mpya ya ukurugenzi wa Sheria na utawala Shirikisho la soka nchini TFF.

Mtawala tayari amewataarifu rasmi Simba kuhusiana na kazi hiyo mpya aliyoipata TFF na viongozi wote wameridhia kuondoka kwenda kusaka changamoto mpya.

Akizungumza na blog ya Supermariotz Mtawala amesema ni kweli ameacha kazi rasmi Simba na amewasilisha barua akiwa tayari pia amezungumza na viongozi wote wa Simba kuhusu maamuzi yake.

"Ni kweli nimeacha kazi Simba nimepata nafasi ya kuwa Mkurugenzi wa Sheria na Utawala wa TFF kazi ambayo naiona ina changamoto mpya na naamini nitaiweza kwa kufuata sheria na kanuni" alisema.

Rais wa TFF Jamal Malinzi anamtambulisha rasmi leo mbele ya waandishi wa habari baada ya mazungumzo yote na Mtawala kukamilika na kukubali kazi hiyo ambayo ni nafasi mpya ya uongozi ndani ya TFF.

Hivi karibuni Mtawala aliapishwa rasmi kuwa mwanasheria.

*www.supermariotz.blogspot.com inampa hongera Mtawala na kumtakia kila la kheri katika kazi yake mpya,tunaamini ni kijana mdogo mwenye uelewa na uwezo mkubwa wa kazi na nafasi hiyo ataimudu.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.