Wednesday, February 19, 2014

Kocha Swansea atoboa siri,ametimuliwa kwa email


Kocha Michael Laudrup amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu kutimuliwam kwake kazi na klabu ya ligi kuu ya Swansea akisema ametimuliwa kwa barua pepe au wazungu wanaita email.

Laudrup amesema alitimuliwa kwa kuambiwa amevunja mkataba na hakupewa nafasi hata ya kuwaaga wachezaji wa kikosi hicho.

Anasema kabla ya kupokea ujumbe huo alikuwa na mazungumzo na wakuu wa Swansea katika kikao ambacho kilimalizika salama na kupeana mikono lakini akashangaa kupokea email ya kibarua chake kuota nyasi kitu ambacho kilimchanganya.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.