Tuesday, April 29, 2014

WAMERUDI : Chelsea vs Atletico Etoo,Terry Hazard,Cech warudi


Chelsea wamepata nguvu kwenye kikosi chao kuelekea mchezo wa kesho wa ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Atletico Madrid baada ya Eden Hazard, Petr Cech, John Terry na Samuel Eto'o kufanya mazoezi ya leo.

Hazard,ambaye Jumapili ametajwa kama mchezaji bora chipukizi na chama cha wachezaji wa kulipwa PFA na Eto'o walikosa mchezo wa kwanza uliomalizika kwa syluhu ya bila kufungana wakati Cech na Terry walitolewa kwa kuumia kwenye mchezo huo wa kwanza uliochezwa Vicente Calderon.

Kupitia mtandao wa kijamii wa twitter ya klabu hiyo umesema kuwa wachezaji hao wote wamehudhuria kwenye mazoezi kwenye viwanja vya Cobham.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.