Wednesday, October 8, 2014

Mayweather sasa amtaka Pacquiao


KAMA ukisoma taarifa ya Jeff Mayweather kaka wa bondia Floyd Mayweather Jr ambayo ameituma inaonesha huenda likapigwa pambano ambalo limepachikwa jina la MEGA FIGHT kati ya Floyd Mayweather na Manny Pacquiao.

Huenda pambano hilo likafanyika mwakani wakati ambao Mayweather ameweka bayana kuwa ataachana rasmi kucheza mchezo huo.

Floyd Mayweather Sr yeye anathibitisha kuwa pambano hilo linaweza kuwepo lakini kama tu Pacquiao raia wa Filipino atashinda pambano lake dhidi ya Chris Algieri.

Mayweather Sr amesema katika pambano hilo anaamini kuwa mtoto wake atashinda kirahisi kama pambano hilo litafanyika.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.