Wednesday, February 4, 2015

Mendes asema Mourinho ndiye mrithi wa Ferguson



Super-agent Jorge Mendes amemwagia sifa mteja wake kocha Jose Mourinho akisema ni yeye pekee mwenye uwezo wa kuchukua utawala wa Sir Alex Ferguson ambaye ameacha historia kubwa kwa timu ya Manchester United.

Ferguson,ambaye alishinda mataji 38 katika miaka 26 aliyokuwepo huko Old Trafford alistaafu mwaka 2013 na nafasi yake ikachukuliwa na David Moyes ambaye hata hivyo alidumu kwa miezi 10 pekee.

Mendes anasema ni ngumu kumpata mtu kama Ferguson kwasababu alikuwa ana akili ya ziada na kumtafuta mtu wa aina hiyo ni ngumu lakini akasema kwa England sasa wana mmoja tu ambaye ni Mourinho.

Anasema Mourinho kwasasa anaweza kufanya hilo kwa Chelsea kwasababu anawapenda mashabiki,anaupenda mji na anafikiri kuwa taka Zaidi ya miaka 10.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.