Monday, December 1, 2014

Aliyempiga Messi kupigwa kifungo cha maisha


Valencia wamesema watamfungia maisha shabiki aliyempiga na chupa ya plastic mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi katika mchezo wao wa jana wa la liga.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 27 alikuwa akishangilia na wenzake bao lilifungwa na Sergio Busquets wakati alipopigwa na chupa hiyo.

Messi hakuumia katika tukio hilo lakini Valencia katika taarifa yake imesikitishwa na kulaani tukio hilo.

Taarifa hiyo imebainisha kuwa klabu hiyo itafanya juhudi kuhakikisha shabiki huyo anakamatwa na kuchukuliwa hatua na atafungiwa maisha kukanyaga Mestalla.

Kocha wa Barcelona Luis Enrique amesema klabu za Hispania zinapigania kuondoka kwa vitendo hivyo vya mashabiki wanaoleta vurugu michezoni.

Mapema katika siku hiyo ya jana shabiki amefariki baada ya kutokea vurugu baina mashabiki kabla ya mchezo wa nyumbani wa Atletico Madrid dhidi ya Deportivo La Coruna.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.