Monday, December 1, 2014

Thierry Henry huyoooo Arsenal,aitema rasmi New York Red Bulls


Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thierry Henry ameitema timu ya New York Red Bulls baada ya kuitumikia kwa miaka minne na nusu kuna ligi kuu ya nchini Marekani MLS.

Mechi ya mwisho kwa mshambuliaji huyo mwenye miaka 37 ilikuwa ni walipotoka sare ya kufungana mabao 2-2 Jumamosi iliyopita hiyo ikiwa na maana Red Bulls wameondolewa kwa jumla ya mabao 4-3 na New England Revolution katika mechi za mtoano za ubingwa wa Eastern Conference.

Henry mwenyewe anasema maamuzi yake tokea awali ilikuwa ni kuondoka baada ya kumaliza muda wake wa mkataba.

Amesema itamchukua wiki chache zijazo kuamua hatima yake ya baadaye.

Hata hivyo taarifa zinasema kuwa Henry anarejea Arsenal katika benchi la ufundi ili kuongeza nguvu kwa washika bunduki hao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.